Header Ads

test

SHAMBULIZI LA KOMPUTA KUATHIRI WATU ZAIDI JUMATATU



Wataalmu wa usalama katika mitandao ya komputa, wanaonya kwamba kunaweza kutokea mashambulio mengine sehemu mbalimbali za dunia, pale watu wataporudi makazini hapo kesho.
Inakisiwa kuwa komputa zaidi ya 120 katika nchi kama 100, zilidukuliwa Ijumaa.
Lakini polisi wa Umoja wa Ulaya wanasema walioathirika ni 200,000 katika nchi 150.
Shambulio hilo limeathiri watumizi pamoja na ofisi za serikali, kampuni zinazotengeneza magari, mabenki na huduma za afya.
Shambulio hilo limezuwia komputa kufikia data, na wanadai kikombozi, ili kuacha kuikorofisha komputa.
Uchambuzi uliofanywa na BBC katika akaunti tatu za sarafu ya kidijitali, bitcoin, unaonyesha washambuliaji wamelipwa kikombozi zaidi ya mara 100, jumla ya dola karibu 30,000.
Source: BBC

Tangaza Nasi kupitia Dawatihurutz.blogspot.com

No comments