Header Ads

test

Anthony Joshua ashinda kwa KO dhidi ya Wladimir Klitschko Wembley

Anthony Joshua vs Wladimir Klitschko.
Bondia wa Uingereza Anthony Joshua jana ameshinda pambano lake dhidi ya Wladimir Klitschko wa Ukraine katika mchezo wa ngumi za uzito wa juu mbele ya mashabiki 90,000 kwenye uwanja wa Wembley nchini Uingereza.


Bondia Wladimir Klitschko akiwa chini baada ya kupigwa ngumi nzito na mpinzani wake Joshua.
Anthony Joshua mwenye umri wa miaka 27 alifanikiwa kumpiga Wladimir Klitschko mwenye umri wa miaka 41 kwa Knocks Out katika raundi ya 11 ya mchezo huo. Kwa matokeo hayo yanamfanya Anthony Joshua kuweza kuitetea na kuweka rekodi zaidi ya kucheza mapambano 19 na kushinda yote 19 kwa Knocks Out. Pia upande wa bondia wa Ukraine Wladimir Klitschko huu unakuwa mpambano wake wa 5 kupoteza katika historia yake ya kucheza ngumi.


Anthony Joshua akishangilia baada ya kumwangusha kwa ngumi Klitschko.
"[Mimi] 19-0, ndani ya miaka mitatu na nusu katika mchezo," Joshua alisema. "Kama nilivyosema, mimi sio mkamilifu, lakini hujaribu. Nafanya juhudi zaidi. Ndivyo ilivyo. Kama nilivyosema, kama hushiriki, hutaweza kujua matokeo."

Joshua vs. Klitschko ubao wa alama za pambano:

R1R2R3R4R5R6R7R8R9R10R11R12TOTAL
Joshua
10
9
10
10
10
8
9
9
10
10
TKO
95
Klitschko
9
10
9
9
9
10
10
10
9
9
94

Tangaza Nasi kupitia Dawatihurutz.blogspot.com

No comments