POLISI SABA WAUAWA KWA RISASI MKOA WA PWANI
Askari saba wa jeshi la polisi waliokuwa katika doria kijiji cha Jaribu mpakani mwa wilaya za Rufiji na Kibiti mkoani Pwani nchini Tanzania waliuawa na watu wasiojulikana kwa kupigwa risasi majira ya saa 12 jioni Aprili 13, 2017.
Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga
alisema kuwa kwa sasa hawezi kuzungumzia tukio hilo kwani ni mapema sana.
Aliwasihi waandishi kumuacha kwanza hadi hapo taarifa rasmi itakapoandaliwa
ataweza kuujulisha umma kuhusu yale yote yaliyotokea.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mwigulu Nchemba
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo licha ya kusema kuwa hana taarifa za
kutosha juu ya tukio zima hadi hapo atakapowasiliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu. Lakini aliahidi kuwa watu hao watatafutwa popote pale walipo na
hatua dhidi yao zitachukuliwa ili kukomesha vitendo hivyo.
Kwa mujibu wa taarifa za awali zinadai kuwa polisi hao walikuwa kwenye gari wakirejea kituoni kutoka kwenye doria na walishambuliwa na watu waliotokea msituni na dereva wa gari
la polisi alipigwa risasi na kupoteza uwezo wa kuongoza gari na kisha askari
wengine waliokuwepo wakashambuliwa. Askari mmoja aliyejeruhiwa amelazwa katika
Hospitali ya Mchukwi.
Tangaza Nasi kupitia [dawatihurutz.blogspot.com]
Post a Comment