Header Ads

test

BREAKING NEWS: KAMATI YA SAA 72 YAIRUDISHA SIMBA MBIO ZA UBINGWA, YAIPA POINTI 3




Kamati ya Ligi ya masaa 72 iliyokaa kikao leo April 13, 2017 na kuamua kuhusu malalamiko ya Simba dhidi ya Kagera Sugar kumtumia mchezaji Mohamed Fakhi katika mchezo wa April, 2 2017 huku akiwa na kadi tatu za njano kinyume na taratibu na kanuni za Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Simba walipeleka malalamiko hayo katika bodi ya Ligi na kuomba ipitie ripoti za waamuzi ili kujulikana ukweli, leo April 13 kamati ya saa 72 chini ya mwenyekiti wake Hamadi Yahaya ilikaa na kujiridhisha kuwa Kagera walikiuka taratibu hizo kwa mujibu wa Kanuni, hivyo ikaamua kuwapa Simba point zote tatu na magoli matatu kutoka  mchezo huo dhidi yao. Simba imefikisha pointi 61 mbele ya wapinzani wao Yanga wenye Pointi 56.

Mohamed Fakhi wa kwanza kushoto.

Kamati imejiridhisha kuwa mchezaji Mohamed Fakhi alioneshwa kadi za njano katika michezo dhidi ya Majimaji, Mbeya City na African Lyon, hivyo hakustahili kucheza katika mchezo dhidi ya Simba uliyochezwa April, 2 2017 katika uwanja wa Kaitaba na Simba ikapoteza kwa magoli 2-1.


Msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya Simba kushinda rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar:







No comments