FREEMAN MBOWE NA HALIMA MDEE WAFIKA KAMATI YA MAADILI YA BUNGE KUHOJIWA
Kiongozi wa kambi ya Upinzani Bungeni (KUB), Mhe. Freeman Mbowe akihojiwa mbele ya kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kufuatia amri ya Mhe. Spika wa Bunge ya kumtaka afike mbele ya kamati hiyo kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kutokana na matamshi yasiyo na staha aliyoyatoa mapema mwezi Machi 2017 Bungeni Mjini Dododma yaliyokuwa na madiya kudharau Bunge. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Mhe. Halima Mdee akihojiwa mbele ya
kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kufuatia amri ya Mhe. Spika wa
Bunge ya kumtaka afike mbele ya kamati hiyo kujibu tuhuma zinazomkabili za
kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kutokana na kutoa kauli ya matusi
Bungeni na kumtukana Spika, matamshi aliyoyatoa mapema mwezi Machi 2017 Bungeni
Mjini Dodoma yaliyokuwa namadai ya kudharau Bunge. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Post a Comment