KAULI ZA RAIS MAGUFULI WAKATI WA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASA DAR ES SALAAM - MOROGORO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa reli ya kisasa standard gauge kutoka jijini Dar es Salaam hadi Morogoro.
Hizi hapa kauli zake katika uzinduzi huo;
'Ujenzi wa reli huwa ni gharama kubwa, reli hii
itakuwa inabeba uzito mkubwa na spidi kubwa, watu watalala Moro na watafanya
kazi DSM'- Rais Magufuli
'Ujenzi wa reli ya kisasa utakuza sekta zingine
nchini, itawezesha malighafi mbalimbali kusafirishwa kwenda kwenye maeneo ya
viwanda'- Rais Magufuli
'Ujenzi wa reli hii ya kisasa utasaidia kutunza
barabara zetu, barabara zetu zinaharibika kwa sababu zinasafirisha mizigo
mikubwa'- Rais Magufuli
'Mradi huu wa ujenzi wa reli ya kisasa
unatarajiwa kutoa ajira kwa watu takribani 600,000'-Rais Magufuli
'Mradi huu wa ujenzi wa reli ya kisasa
unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 30'-Rais Magufuli
'Wale wataalamu wa kusoma kwenye mitandao
wakaangalie ni nchi gani imejenga reli ya namna hii kwa pesa zake watakuta ni
Tanzania'- Rais Magufuli
'Unapokuwa dereva wa lori na unapopakia abiria
hutakiwi kuwauliza wasimame waangalie sehemu gani, dereva mzuri anangalia
kufika salama'- Rais Magufuli
'Nawahakikishia Watanzania mimi ni dereva mzuri
nawahakikishia lori litafika kule tunakokwenda na hili ni lori la maendeleo'- Rais Magufuli
'Kazi tunazozifanya mara nyingi utakaowaona
wanapiga kelele ni wale ambao walizoea kupiga dili, na mimi nataka waendelee
kupiga kelele'- Rais Magufuli
'Tanzania imekuwa kwa uchumi 7%, ushahidi wa
kukua kwa uchumi ndio hii miundombinu tunayoijenga'- Rais Magufuli
'Hivi karibuni tumepata mkopo wa kuanza kujenga
barabara za mwendokasi katika awamu ya tatu na ya nne'-Rais Magufuli
'Tunajua tunapoenda pasitokee mtu wa
kubadilisha ajenda tuanze kuzungumzia ajenda ambazo hazipo kwenye ilani ya
uchaguzi'-Rais Magufuli
'Nataka mhandisi amalize mradi wa reli ya
kisasa kabla ya miezi 30, na ikiwezekana siku ya kufungua twende bure mpaka
Dodoma'-Rais Magufuli
'Vita ya kupambana na ufisadi ni ngumu na hasa
unapowabadilisha watu wachache waliozoea maisha fulani kwa miaka 50'-Rais
Magufuli
'Wanasema samaki mkunje akiwa mbichi, fisadi
mkunje akiwa mbichi akishakomaa mvunje, nafuu walalamike wachache, Watanzania
wafurahi'- Rais Magufuli
'Nazuia hata michanga ya madini, ninafanya kazi
hii kwa niaba yenu, kwani nashindwa kusema nipelekee hiyo michanga nitaikuta
Ulaya?'- Rais Magufuli
'Mlinituma nifanye haya, au niwaulize ndugu
zangu haya yote ninayoyafanya kweli ni mabaya?'- Rais Magufuli
'Niko kwa niaba yenu, tumeonewa sana, Tanzania
ni tajiri hatutakiwi kuwa ombaomba'- Rais Magufuli
'Tanzania tunaweza kwa hiyo tunapoyafanya haya
tunafanya kwa sababu tuna wajibu wa kufanya, na haya ni malipo yangu
kwenu'-Rais Magufuli
'Watanzania wanataka maendeleo, hakuna
anayekula siasa kwa hiyo Tanzania kwanza siasa baadae'-Rais Magufuli
'Niwaombe tuangalie Tanzania kwanza siasa baadae,
muiache Serikali ya CCM iliyoaminiwa na Watanzania itekeleze wajibu wake
tutakutana 2020'- Rais Magufuli
Post a Comment